1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaLebanon

UN yatoa wito kwa Israel na Hezbollah kusitisha mvutano

21 Septemba 2024

Afisa mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya kisiasa Rosemary DiCarlo amezihimiza nchi zote zilizo na ushawishi juu ya Israel na kundi la Hezbollah kutumia ushawishi huo kuzirai pande hizo kusitisha mvutano.

https://p.dw.com/p/4kvBc
UN - Rosemary DiCarlo
Afisa mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya kisiasa Rosemary DiCarloPicha: Eskinder Debebe/Xinhua News Agency/picture alliance

Bi Rosemary ametahadharisha kuwa iwapo vita kamili vitatokea kati ya Israel na Hezbollah huenda vikasababisha uharibifu mkubwa zaidi kuliko ule ulioshuhudiwa hadi sasa.

Ametoa rai hiyo kwa wajumbe wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa baada ya kulipuka kwa vifaa vya mawasiliano vya Hezbollah ambapo watu 37 waliuawa na maelfu ya wengine kujeruhiwa.

Soma pia:  Hizbullah, Israel washambuliana vikali

Waziri wa mambo ya nje wa Lebanon Abdallah Bou Habib ameilaumu Israel kwa kuhusika na hujuma hiyo na kuongeza kuwa hakuna mtu yoyote duniani aliye salama.

Balozi wa Israel katika Umoja wa Mataifa Danny Danon amesema nchi hiyo haina nia ya kuutanua mzozo katika eneo la Mashariki ya Kati lakini haitaruhusu kundi la Hezbollah kuendelea na uchokozi wake.