1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Putin akutana na naibu waziri mkuu wa Serbia

4 Septemba 2024

Rais wa Urusi Vladmir Putin amekutana na naibu waziri mkuu wa Serbia leo katika mji wa Vladivostok nchini Urusi, pembezoni mwa jukwaa la kiuchumi linalohudhuriwa na Putin.

https://p.dw.com/p/4kHM0
Urusi | Rais Vladimir Putin
Rais wa Urusi Vladimir PutinPicha: Vyacheslav Prokofyev/Sputnik/REUTERS

 Mkutano wa viongozi hao unafanyika wiki moja baada ya serikali ya mjini Belgrade kusaini mkataba wa mabilioni ya dola wa ndege za kivita na Ufaransa.

Naibu waziri mkuu wa Serbia Aleksander Vulin amesema nchi yake haiwezi kuwa mwanachama wa jumuiya ya kujihami ya NATO, lakini pia haitothubutu kuiwekea vikwazo Urusi na pia haitoiruhusu kutumiwa katika hatua zozote dhidi ya Urusi.

Soma pia:Serbia yamuahidi Putin kwamba kamwe haitaigeuzia mgongo

Urusi na Serbia zina mahusiano ya karibu kihistoria. Nchi hiyo pia imeendelea kujitenga na Umoja wa Ulaya katika hatua za kuiwekea vikwazo Urusi kuhusiana na vita vya Ukraine.


 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW