1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MichezoUfaransa

Ni Real dhidi ya Chelsea, Guardiola kuikabili Bayern

17 Machi 2023

Mabingwa watetezi Real Madrid watacheza dhidi ya washindi wa mwaka wa 2021 Chelsea katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

https://p.dw.com/p/4OqWT
FC Bayern trifft auf Manchester City
Picha: Martial Trezzini/Keystone/dpa/picture alliance

Mabingwa watetezi Real Madrid watacheza dhidi ya washindi wa mwaka wa 2021 Chelsea katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Pep Guardiola na Manchester City yake atakutana a klabu yake ya zamani Bayern Munich baada ya droo iliyofanywa leo mjini Nyon. Mabingwa watetezi wa Italia AC Milan watacheza dhidi ya mabingwa watarajiwa wa msimu huu Napoli katika mechi inayozikutanisha timu mbili za Italia, wakati Inter Milan itakabana koo na Benfica ya Ureno. Mechi za mkondo wa kwanza zitachezwa Aprili 11 na 12 wakati mkondo wa pili utakuwa Aprili 18 na 19.