1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jeshi la Congo na MONUSCO watangaza operesheni ya pamoja

Angela Mdungu
4 Novemba 2023

Wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo - MONUSCO wametangaza operesheni ya pamoja na jeshi la kitaifa, inayolenga kuwazuia waasi wa M23 kuikamata miji muhimu ya mashariki.

https://p.dw.com/p/4YOlW
DR Kongo | MONUSCO | Unrühen
Askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini DRC-MONUSCOPicha: Moses Sawasawa/AP Photo/picture alliance

Tangazo hilo linafuatia kuongezeka kwa makabiliano na kundi la M23 tangu mwezi uliopita, ambayo yamewalazimu watu 200,000 kuyakimbia makazi yao kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, baada ya kushuhudiwa kipindi cha utulivu.

Hili pia limejiri baada ya serikali ya Congo kuomba jeshi hilo liondoke. Akiwahutubia waandishi habari katika mji wa mashariki wa Goma, Kamanda Mkuu wa Jeshi la MONUSCO  Otavio Rodrigues de Miranda Filho alisema kuongezeka kwa machafuko katika siku za karibuni kunatia wasiwasi.

Alifafanua kuwa operesheni mpya ya kijeshi ya pamoja na jeshi la Congo, ilinayoitwa Springbok italenga kulinda mji wa Goma na mji ulio karibu wa Sake. Miranda Filho amesema M23 sasa inasonga mbele kuelekea Sake.