1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaHaiti

Haiti yaunda baraza la mpito la uchaguzi wa mwaka 2026

19 Septemba 2024

Serikali ya Haiti imeunda baraza la mpito la uchaguzi, ikiwa ni hatua ya mwanzo kuelekea kufanyika uchaguzi ifikapo mwaka 2026.

https://p.dw.com/p/4kpBT
Michel Martelly I Rais wa Haiti
Aliyekuwa rais wa Haiti, Michel Martelly, akizungumza Julai 17, 2011 huko Port-au-Prince.Picha: Soeren Stache/dpa/picture alliance

Ofisi ya Waziri mkuu imesema baraza hilo la mpito lililoundwa jana tayari lina viti saba vinavyowakilisha makundi ya kidini, waandishi wa habari, wakulima na vyama vya wafanyikazi.Hata hivyo viti vyengine viwili – kimoja cha mashirika ya haki za binadamu na kingine kwa ajili ya makundi ya wanawake, bado havina mwakilishi. Nchi hiyo yaCaribbean ilifanya uchaguzi mkuu mara ya mwisho mnamo mwaka 2016. Kwa kawaida, uchaguzi unafaa kufanyika kila baada ya miaka mitano lakini kutokana na hali ya kisiasa kuwa tete na kufuatia ombwe la madaraka lililosababishwa na kuuawa kwa Rais Jovenel Moise mwaka 2021, tangu wakati huo nchi hiyo imekuwa bila rais. Makundi yenye silaha yametanua udhibiti wao na sasa yanatawala takriban asilimia 80 ya mji mkuu wa Port-au-Prince na maeneo mengine ya taifa hilo.